MICHEZO

Klabu ya soka nchini uingereza ARSENAL imeenamisha kichwa chini baada ya kufanyiwa ukatili wa kufungwa mabao matatu kwa moja ktk na timu ya chelsea, mabao ya chelsea yalifungwa mnamo dakika ya 13 na mchezaji M.Alonso raia wa uhispania bao la pili lilifungwa dk 53 na mchezaji E.Hazard goli la mwisho la chelsea likifungwa na C.Fabrigas ktk dk ya 85 nalo goli la kufutia machozi la klabu ya Arsenal lilifungwa na O.Giroud mnamo dk ya 90+1 akitokea bench.
Michezo mingine ilikuwa ni kati ya Cristal pales akichuana na sanderland ambapo sanderland ilipata ushindi mpana wa mabao manne kwa bila mabao yakifungwa na L.Kone dk 9,D.Ndong dk ya 43, J.Defoe 45+1 na lamwisho akamalizia huyohuyo dk 45+3
kwa upande wa everton iliibuka na ushindi wa mabao 6 kwa 3 dhidi ya bournemouth,hull city 2-0 liverpool, southampton 1-3 west ham united,watford 2-1 burney, tottenham hotspor 1-0 middlesbrough 
Mpaka kukamilika michezo ya jana chelsea inaendelea kushika nafasi yake ya kwanza akiwa na alama 59 alama 9 mbele dhidi ya tottenham anaeshika nafasi ya pili akiwa na alama 50.
Leo kutapigwa michezo miwili pekee Manchester City VS Swansea City 9:30 jioni
Leicester City VS Manchester United 1:00 jion

Chapisha Maoni

0 Maoni

Sheikh Nyundo